You are currently viewing Kaa La Moto aachia rasmi Album yake mpya

Kaa La Moto aachia rasmi Album yake mpya

Rapa kutoka Kenya Kaa La Moto ameachia rasmi Album yake mpya, inayokwenda kwa jina la “Mkanda Mweusi.”

Album hiyo, ina jumla ya mikwaju 15 huku ndani akiwapa shavu wakali kama AY, Joh Makini, Dully Sykes, Kala Jeremiah, Johnny Skani, Jua Cali, Kelechi Africana na wengine wengi.

Hata hivyo  Mkanda Mweusi Album inapatikana Exclusive kwenye majukwaa yote ya kupakua na kusikiliza muziki mtandaoni.

Hii itakuwa ni album ya pili kutoka kwake mwaka huu ikizingatiwa kuwa mwezi Mei aliachia Album iitwayo “Leso ya Mekatilili” iliyokuwa na jumla ya nyimbo 12.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke