You are currently viewing Kaa La Moto aachia Tracklist ya Album yake mpya

Kaa La Moto aachia Tracklist ya Album yake mpya

Rapa kutoka Kenya Kaa La Moto ameachia Tracklist ya Album yake mpya, inayokwenda kwa jina la Mkanda Mweusi.

Album hiyo, ina jumla ya mikwaju 15 huku ndani akiwapa shavu wakali kama AY, Joh Makini, Dully Sykes, Kala Jeremiah, Johnny Skani, Jua Cali, Kelechi Africana na wengine wengi.

Hata hivyo amewataka mashabiki zake kukaa mkao wa kula kupokea Mkanda Mweusi Album,  ambayo itaingia sokoni rasmi Disemba 20 mwaka huu.

Hii itakuwa ni album ya pili kutoka kwa mtu mzima Kaa La Moto kwa mwaka huu ikizingatiwa kuwa mwezi mei mwaka huu aliachia Album iitwayo Leso ya Mekatilili iliyokuwa na jumla ya nyimbo 12.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke