You are currently viewing KABAKO ASITISHA GHAFLA ONESHO LAKE HUKO KYENJONJO UGANDA

KABAKO ASITISHA GHAFLA ONESHO LAKE HUKO KYENJONJO UGANDA

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Kabako anakadiria hasara ya maelfu ya pesa baada ya kusitisha onesho lake huko Kyenjonjo kutokana na kushindwa kutumiza maagizo aliyopewa na polisi.

Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Kabako amesema polisi walimkatishia tamaa baada ya kumtoza pesa nyingi ili wampe ruhusa ya kuandaa onesho hilo, jambo ambalo amedai lilikuwa nje ya uwezo wake kwani angeweza kumudu gharama hiyo.

Msanii huyo amewaomba radhi mashabiki zake kwa kukosa kuandaa show yake kama ilivyoratibiwa huku akisema kwamba amefilisika kiuchumi kwa sababu alitumia pesa nyingi kuwalipa wasanii na kuipigia ubatu onesho lake hilo ambalo amelisitisha baada ya kupata vikwazo kutoka kwa polisi.

Hata hivyo Kabako ambaye ameonekana kuumizwa na kitendo cha kusitisha show yake ametoa wito kwa maafisa wa usalama nchini Uganda kufanya mageuzi kwenye baadhi ya sera zao kwani zimekuwa kizingiti kwa wasanii kuandaa matamasha yao ya muziki kutokana na polisi kuwatoza pesa nyingi wanapotaka kuwapaa vibali.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke