You are currently viewing KALIFAH AGANAGA ADAI WAGANDA HAWANA UWEZO WA KUSHINDANA NA WASANII WA NIGERIA

KALIFAH AGANAGA ADAI WAGANDA HAWANA UWEZO WA KUSHINDANA NA WASANII WA NIGERIA

Msanii Kalifah Aganaga amedai kwamba wasanii wa Uganda hawana uwezo wa kushinda kisanaa na wenzao kutoka Nigeria.

Bosi huyo wa Bad Character Records amesema tasnia ya muziki nchini humo imekosa wawekezaji wa kuupeleka muziki wao kwenye soko la kimataifa.

Aganaga amesisitiza kuwa nchi ya Nigeria ina wawekezaji wengi ambao wanatumia mabillioni ya fedha kutanua wigo wa wasanii wao kutambulika kimataifa.

Kauli ya Kalifah Aganaga inakuja baada ya baadhi ya wasanii kutoa lalama zao kwa serikali kuweka mikakati ya kuwashinikiza mapromota wa muziki kuwapa kipau mbele wasanii wa ndani kwenye matamasha yao ya muziki tofauti na wasanii wa kigeni.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke