Rapa Kanye West ameripotiwa kumfukuza kazi mfanyakazi wake kwenye kampuni ya Yeezy kufuatia kupiga wimbo wa Drake ofisini. Hii ni kwa mujibu wa Rolling Stone.
Utakumbuka juzi kati Drake alitapika nyongo kwenye “Circo Loco” ngoma ambayo inapatikana kwenye Album ya pamoja na 21 Savage, Her Loss. Drizzy alifunguka ya moyoni kwamba aliamua kupatana na Kanye West na kufanya onesho la pamoja (Free Larry Hoover Concert) Disemba 10, 2021 kwa sababu ya heshima tu ya godfather wake, J. Prince.
“Linking with the opps, b*tch, I did that shit for J Prince. B*tch, I did it for the mob ties” – alichana Drizzy.