Rapa Kanye West amefikia uamuzi wa kuvunja mkataba wake na kampuni ya GAP baada ya miaka miwili.
YE ameandika barua ya kuvunja mkataba huo kufuatia madai kwamba GAP wameshindwa kutimiza makubaliano ya mkataba wao ambayo walitakiwa kufungua maduka ya Yeezy na kuachia bidhaa za mavazi.
Mwaka 2020 Kanye West alisaini mkataba huo wa ushirikiano wa kibiashara na kampuni ya GAP ambao ulikuwa wa miaka 10.