You are currently viewing KING KAKA AACHIA RASMI COVER YA HAPPY HOUR EP

KING KAKA AACHIA RASMI COVER YA HAPPY HOUR EP

Mkali wa muziki wa Hiphop nchini King Kaka ameachia rasmi Cover  ya EP yake ijayo iinayokwenda kwa jina la “Happy Hour”

Kupitia ukurasa wake instagram King Kaka ametuonyesha cover ya EP yake mpya huku akiwataka mashabiki zake wakae mkao wa kula kuipokea EP hiyo.

Licha ya kuweka wazi jina na cover ya album yake mpya, King Kaka hajatuambia idadi ya ngoma zitakazopatikana kwenye EP hiyo ilia inatarajiwa kuingia sokoni Novemba 30 mwaka huu.

Ikumbukwe Happy Hour EP kutoka kwa mtu mzima King Kaka ilipaswa kuachiwa rasmi  Oktoba mosi mwaka huu lakini ilishindikana kutokana na King Kaka kujikita kwenye kuiweka sawa afya yake baada ya kuugua kwa kipindi cha miezi minne iliyopita.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke