Mwanamuziki kutoka Uganda King Saha amejiongezea usalama baada ya kujitangaza rais mpya wa chama cha wanamuziki Uganda.
Hitmaker huyo wa ngoma ya “Zakayo” amesema amechukua hatua hiyo kutokana na wadhfa huo wa urais kumweka kwenye hatari ya kushambuliwa na wahuni.
Msanii huyo aidha amekanusha madai yanayotembea mtandaoni kwamba alikodisha walinzi kwa hofu ya kushambulia na hasimu wake Bebe Cool ambaye wamekuwa kwenye bifu kwa muda sasa.
King Saha alijitangaza kuwa rais wa chama wa wanamuziki uganda baada ya Cindy Sanyu ambaye ni rais wa sasa wa UMA kuendelea na majukumu yake akidai kuwa kuna pengo la uongozi katika chama hicho.