You are currently viewing KRG THE DON AFUNGUA SHAURI LA TALAKA MAHAKAMANI

KRG THE DON AFUNGUA SHAURI LA TALAKA MAHAKAMANI

Msanii wa muziki wa dancehall nchini KRG The Don amefungua shauri la talaka mahakamani dhidi ya mke wake Linah Wanjiru, shauri hilo limefunguliwa katika Mahakama ya Milimani Jijini Nairobi.

KRG ameweka wazi hilo kupitia instagram page yake baada ya kupost  nyaraka za kisheria kuhusiana na mchakato wa talaka na kusindikiza na caption inayosomeka “kwa wale waliyokuwa wanachukulia kwa mzaha, poleni”

Hitmaker huyo Giddem alifunga ndoa na mke wake huyo mwaka wa 2014 na wamejaliwa kupata wawili kwa pamoja.

Hatua ya KRG kufungua shauri la talaka dhidi mke wake inakuja siku chache baada ya kumsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke