You are currently viewing KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

Baada ya uvumi wa wiki kadhaa,  Msanii wa muziki wa Dancehall nchini KRG The Don hatimaye amethibitisha kuwa yeye na mke wake sio wapenzi tena.

KRG ameweka wazi hilo kupitia Instagram page yake baada ya kupost picha ya mke wake huyo na kusindikiza na caption inayoashiria kuwa wameachana rasmi.

Hitmaker huyo “Giddem” amemsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao.

KRG pia ametumia fursa hiyo kukanusha madai yanayosambaa kwenye mitandao kuwa alitoka nje ya ndoa yake na ndio maana uhusiano wake na Baby mama wake ulivunjika.

Hata  hivyo, bado haijabainika kama kuna ukweli wowote kuhusu stori za wawili hao kuachana ila kwa sasa wamefuta picha zote walizowahi kupiga wakiwa pamoja kwenye mtandao wa Instagram.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke