You are currently viewing KUMBE THE GAME ALIMTUPIA JAY Z MATUSI MAZITO BAADA YA KUMNYIMA NAFASI YA KUTUMBUIZA KWENYE SUPER BOWL 2022

KUMBE THE GAME ALIMTUPIA JAY Z MATUSI MAZITO BAADA YA KUMNYIMA NAFASI YA KUTUMBUIZA KWENYE SUPER BOWL 2022

Rapa The Game kutoka Marekani amekasirika sana baada ya kukosa nafasi ya kutumbuiza kwenye Halftime show ya Super Bowl 2022, Wiki iliyopita alitokwa mapovu na kusema 50 Cent hakustahili kupewa nafasi hiyo.

Meneja wake aitwaye Wack 100 ameibuka na kutusanua makubwa ambayo hatuyafahamu nyuma ya pazia. Wack 100 amesema The Game alimtukana Jay-Z tusi zito “Suck My D**k” baada ya kumnyima nafasi ya kutumbuiza kwenye Halftime show ya fainali hizo za mwaka huu.

Utakumbuka Roc Nation ya Jay Z waliingia makubaliano na NFL kuwa waandaaji wa burudani kwenye Super Bowl 2022.

Kinyongo baina ya wasanii hao kilianza mwaka 2005 baada ya The Game kudai kwamba alijibiwa vibaya na Jay-Z walipokutana kwenye mgahawa wa 40/40 mjini New York ambapo The Game alimuomba ushauri Jigga ya namna ya kudumu muda mrefu kwenye muziki.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke