You are currently viewing KUNDI LA B2C LAMCHANA BEBE COOL KWA MADAI YA KUUKOSOA WIMBO WA AMAPIANO

KUNDI LA B2C LAMCHANA BEBE COOL KWA MADAI YA KUUKOSOA WIMBO WA AMAPIANO

Wasanii wa kundi la B2C Boys wamemtolea uvivu  Bebe Cool kwa kuiponda wimbo wao uitwao “It’s Okay” ambao wameimba kwa mtindo wa amapiano.

Wasanii hao wamemtaka Bebe Cool kukoma kuingilia mambo yao na badala yake aelekeze nguvu zake kwenye suala la kuboresha muziki wake.

“Hawezi kufikiria kwa ajili yetu. Njia yake ya kufanya mambo sio sawa na yetu. Hatuwezi tu kupata pesa kupitia harusi. Tulifanya amapiano kulenga soko la kimataifa na tumefaidika,” watatu hao walieleza.

Ikumbukwe Bebe Cool alisema kuwa  kundi la B2C wanaua brand zao na kupoteza rasilimali kwa kufanya mtindo huo wa muziki. Alienda mbali zaidi na kusema kuwa hawatapewa nafasi ya kutumbuiza wimbo huo kwenye sherehe za harusi kutokana na ubovu wa wimbo huo.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke