Label ya Atlantic Records imejipata pabaya kufuatia tuhuma za kutumia Robots kutengeneza views YouTube kwenye video mpya za wasanii wake Lil Uzi Vert, Roddy Ricch, A Boogie na Don Toliver. Wadau mbali mbali wa muziki duniani wameisuta vikali Label hiyo wakisema inajishusha kisanaa.
Aidha kwa taarifa iliyotolewa na tovuti ya TMZ usiku wa kuamkia leo, Atlantic Records imekanusha kufanya mchezo huo mchafu
“Atlantic Records has never used bots for any of our artists.”