You are currently viewing Lady Mariam akanusha madai ya kustaafu muziki

Lady Mariam akanusha madai ya kustaafu muziki

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini uganda Lady Mariam amepuzilia mbali madai ya kuchukua mapumziko kwenye muziki wake.

Hitmaker huyo wa “Tindatine” amesema bado anajishughulisha na masuala ya uimbaji ila kwa sasa anahitaji mtu ambaye atawekeza kwenye muziki wake kwa kuwa muziki umebadilika pakubwa.

“Sijawahi kuacha muziki kama watu wengi wanavyodhani. Bado naimba lakini nahitaji mtu wa kuwekeza katika taaluma yangu kwa sababu muziki umebadilika sana,” alieleza katika mahojiano.

Lady Mariam ambaye ana kiu ya kurudi kwenye game ya muziki Afrika Mashariki, juzi kati alitoa rai kwa mapromota wamzingatie kwenye shows zao kwani bado ana uwezo wa kutoa burudani kwa mashabiki.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke