You are currently viewing Lupita Nyongo amtambulisha mpenzi wake kwa dunia

Lupita Nyongo amtambulisha mpenzi wake kwa dunia

Nyota wa Filamu nchini Lupita Nyongo ameweka wazi kuwa anachumbiana na mpenzi wake ambaye ni ripota wa michezo na muasisi mwenza wa kampuni ya mavazi ya Surfapparel Company ,Selema Masekela.

Lupita amethibitisha habari hiyo njema kwa mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuposti video hii na kisha akaambatanisha na maneno yanayosomeka, “We just click! @selema #thisismylove #nuffsaid

Hata hivyo mashabiki na mastaa mbali mbali wamempongezwa kwa hatua hiyo kubwa maishani huku wakiwataka kila la kheri katika safari yao mpya ya mapenzi.

Utakumbuka Lupita Nyongo hajakuwa na mazoea ya kuanika mambo yake ya mahusiano mtandaoni ila kumekuwa na tetesi kuwa huenda mrembo huyo aliwahi kuwa penzni na mwigizaji wa filamu maarufu ya “Black Panther” Chadwick Boseman aliyefariki Agosti 28 mwaka 2020 kutokana na saratani ya utumbo.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke