You are currently viewing LYDIA JAZMINE AFUNGUKA CHANZO CHA UKIMYA WAKE KWENYE MUZIKI

LYDIA JAZMINE AFUNGUKA CHANZO CHA UKIMYA WAKE KWENYE MUZIKI

Ni takribani miezi tano imepita kutoka staa wa muziki nchini uganda Lydia Jazmine aachie wimbo wake uitwao “Kapeesa”

Ukimya wa  Lydia Jazmine  kwenye muziki umekuwa na maswali mengi sana kwa mashabiki na wadau wa muziki nchini Uganda.

Sasa  kwenye mahojiano yake hivi karibuni Lydia Jazmine   ameweka wazi sababu zilizofanya akae kimya kwa miezi hiyo yote huku utaratibu wake wa kuachia nyimbo kwa miaka miwili ukiwa wa kusuasua.

Lydia Jazmine ameweka wazi kuwa alikuwa anasumbuliwa na tatizo la  vidonda vya tumbo ulcers kwa zaidi ya miezi tano ila kwa sasa anamshukuru mungu amepona.

Mrembo huyo ameweka wazi hilo alipokuwa anatambulisha wimbo wake mpya uitwao “Tonkoseza” ambapo amewataka mashabiki zake kukaa mkao kupokea nyimbo zake ambazo atakuwa anaachia back to back.

 

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke