You are currently viewing Marapa Quavo na Take Off wamkataa Cardi B

Marapa Quavo na Take Off wamkataa Cardi B

Marapa Quavo Huncho na Take Off kutoka Marekani wamemkataa aliyekuwa shemeji yao Cardi B ambaye ni Baby Mama wa Offset aliyekuwa anaunda kundi la Migos.

Wawili hao baada ya kuulizwa kwenye mahojiano na Drink Champs kuwa wapo upande upi kati ya Cardi B na Nick Minaji Take Off Bila kusita alimtaja Nicki Minaj.

Kauli hii imezua mijadala kwa mashabiki wengi wakidai kuwa jamaa wameamua kumkomesha Cardi B maksudi kufuatia kuvunjika kwa kundi la Migos kwani inaaminika kuwa Cardi B ndiye alimshawishi kimapenzi Mume wake Offset ajiondoe kwenye kundi la Migos.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke