You are currently viewing Mashabiki zangu wengi wanaume – Maua Sama

Mashabiki zangu wengi wanaume – Maua Sama

Msanii wa Bongo Fleva, Maua Sama amedai mashabiki wake wengi ni wanaume na ndio maana imekuwa vigumu kwake kudumu kwenye mahusiano.

Hata hivyo, tangu amekuwa maarufu kupitia muziki, Maua Sama hajawahi kuweka wazi mahusiano yake licha ya kuandamwa na tetesi za hapa na pale.

“Mashabiki zangu wengi wanaume, ndio maana maboyfriend hawakai, huko kwenu vipi mnavumiliana?,” Maua Sama ameandika Twitter.

Kwa sasa Maua Sama anafanya vizuri na remix ya wimbo wa Mwana FA, Sio Kwa Ubaya

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke