You are currently viewing MAUA SAMA AFUNGUKA KUACHIA NGOMA BACK TO BACK

MAUA SAMA AFUNGUKA KUACHIA NGOMA BACK TO BACK

Baada ya kuwa na muendelezo mzuri wa kuachia ngoma back to back ambapo tayari ana mwezi mmoja tangu aachie smash hit yake ya ‘Zai’, Maua Sama ana kazi nyingine mpya ambayo ni ‘Baba Jeni’, na kupitia taarifa yake kwa umma ameeleza kwanini anaachia kazi hivyo.

Msanii huyo amebainisha kuwa hiyo ni staili tu ya kutoa muziki wake ambayo ameipa jina la “Uzazi wa mpango wa muziki” yaani mtoto akienda mjini anamleta mwengine, huku akiwataka mashabiki waendelee kuwa wavumilivu.

Hata hivyo ngoma hizo ambazo Maua sama amekuwa akiachia siku za hivi karibuni zimekuwa zikifanya vizuri sana.

Ikumbukwe Maua Sama ni miongoni mwa wasanii wakike wanaofanya vizuri nchini Tanzania tangu alipoibuka miaka minne iliyopita akiwa na mkali wa rap Mwana f.a ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Muheza mkoani Tanga.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke