You are currently viewing MAUA SAMA ATAJWA KUWANIA TUZO ZA NEW VISION INTERNATIONAL AWARDS

MAUA SAMA ATAJWA KUWANIA TUZO ZA NEW VISION INTERNATIONAL AWARDS

Hakika huu ni mwaka wenye neema kwa msanii Maua Sama kwasababu licha ya ngoma zake kufanya vizuri kupitia digital platforms mbalimbali, kubwa zaidi ni kuwa miongoni mwa watakaowania kwenye tuzo za nchini Uholanzi.

Maua ametajwa kuwania tuzo ya video bora ya mwaka kupitia video ya ZAI kwenye tuzo za “New Vision International Awards” (NVIFF) huko Amsterdam nchini Uholanzi.

Video hiyo ya Zai ambayo ina mwezi mmoja tangu ipandishwe Youtube, hadi sasa ina zaidi ya views 796K kwenye chaneli rasmi ya Maua Sama.

Tuzo hizo za nchini Uholanzi zinatarajiwa kutolewa Desemba 20, 2021.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke