You are currently viewing MAUA SAMA ATAMANI KUINGIA KWENYE NDOA

MAUA SAMA ATAMANI KUINGIA KWENYE NDOA

Huenda tukio la Harmonize kumvisha Kajala pete ya uchumba limemgusa pakubwa mwimbaji wa bongofleva maua sama akitamani kuwa kwenye mahusiano, kwani ametangaza kuwa yupo single.

Maua ametumia neno “Jimbo Lipo Wazi” akiwa na maana kwamba hayupo kwenye mahusiano kama ambavyo ujumbe huo unavyomaanisha huko mitaani.

Maua sama ameandika “JIMBO LIPO WAZI ” akiwa ameambatanisha na emoji ya pete pamoja na pilipili.

Hata hivyo kwenye post hiyo ya maua sama upande wa comments, mashabiki wake wanaonekana kutokubaliana nae kwa hilo wakiamini yupo mwenye jimbo lake.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke