Nyota wa muziki wa Bongofleva, Mbosso ambaye kwa sasa anafanya vizuri na EP yake mpya, amesitisha ziara (tour) yake ya muziki nchini Marekani hadi tarehe mpya zitakapotangazwa tena.
Marekani ambayo ilitarajiwa kuanza Novemba 25 mpaka Desemba 16, 2022.
Kupitia instastory ya Mbosso metoa sababu za Kusitisha Ziara yake ya kwa kusema kuwa Daktari amemtaka kutokusafiri au kukaa kwenye Ndege kwa zaidi ya Masaa nane.
Mbali na hayo Mbosso ameahidi kuwa Tour hiyo itaendelea pindi atakapo pata ruhusa kutoka kwaa Daktari..
Itakumbukwa, ziara (tour) hiyo ya Mbosso ilitakiwa kuanza rasmi mwezi huu, tarehe 25 na kumalizika Desemba 16.