You are currently viewing Mejja ahapa kutoanika mahusiano yake kwenye mitandao ya kijamii

Mejja ahapa kutoanika mahusiano yake kwenye mitandao ya kijamii

Staa wa muziki nchini Mejja amefunguka kuwa hatokuja kuweka wazi mahusiano yake kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano yake hivi karibuni hitmaker huyo wa “Kanairo Dating” amesema ameamua kuchukua hatua hiyo kwa sababu mahusiano yake ya nyuma yalikumbwa na mikosi kutokana yeye kuanika mtandaoni.

Mejja ambaye amethibitisha kuwa kwenye mahusiano mapya ya kimapenzi amesema hana mpango wa kumchumbia mtu maarufu hasa msanii mwenzake kwani mastaa wengi huwa hayadumu kwenye mahusiano.

Utakumbuka Mejja alikuwa kwenye mahusiano na mrembo aitwaye Milly Wairimu lakini walikuja wakaachana kwa madai ya usaliti.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke