Mwimbaji mpya ndani ya lebo ya King’s Music Vanillah music aliyetambulishwa rasmi Novemba 3 mwaka huu na lebo hiyo, ameianza safari yake ya muziki akiwa na King’s Music kwa kuachia EP iitwayo “Listen To Me” yenye jumla ya ngoma 6.
“Listen To Me” EP ina nyimbo kama Unanisitiri, Utachuma, Chizi, Nilimpemda Sana, Ananipigiania, Ayee na inapatikana kupitia digital plaforms zote za kuisikiliza mitandaoni.
Kings Music kwa mwaka sasa imekuwa chini ya wasanii wanne; AliKiba, K2GA, Abdu Kiba na Tommy Flavour, hii ni baada ya kuondokewa na wasanii wawili, Killy na Cheed.