You are currently viewing Msanii wa zamani wa Jungle Masters Lypso wa Cate afariki dunia

Msanii wa zamani wa Jungle Masters Lypso wa Cate afariki dunia

Aliyekuwa msanii wa Junge Masters Lypso  amefariki dunia usiku wa kuamkia Novemba 17, 2022 kaunti ya Nairobi.

Taarifa hiyo imethibitisha na rafiki yake wa muda mrefu Dogo Richie ambaye amesema msanii huyo alianguka ghafla akiwa bafuni na kufariki papo hapo.

Kwa mujibu wa Dogo Richie mipango ya kumpumzisha Lypso kwenye nyumba yake ya milele inaendelea huku akiwataka mashabiki kuiweka familia yake kwa maombi wakati huu mgumu.

Lypso ambaye amemuacha mke na mtoto mmoja, enzi za uhai wake aliwahi kutamba na nyimbo kama Size Yangu, Samantha na nyingine nyingi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke