You are currently viewing Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil Neymar kukosa mechi mbili

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil Neymar kukosa mechi mbili

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil Neymar hatashiriki mechi mbili zijazo za Brazil za Kombe la Dunia (Switzerland & Cameroon) baada ya kupata jeraha sehemu ya fundo la mguu wa kulia, kwa mujibu wa taarifa toka kwa daktari wa timu yao.

Mshambuliaji huyo aliondolewa uwanjani dakika ya 80 ya mchezo wa siku ya Alhamisi ambapo Brazil waliichapa Serbia 2-0 baada ya kukabiliwa vikali na Nikola Milenkovic.

Hivyo Neymar anatarajiwa kurejea uwanjani katika hatua ya mtoano ikiwa Mabingwa hao mara 5 wa kombe la Dunia watafuzu kwenda hatua hiyo

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke