You are currently viewing MUONEKANO WA NADIA MUKAMI WAZUA  GUMZO MTANDAONI, ADAIWA ANA UJA UZITO WA ARROW BOY

MUONEKANO WA NADIA MUKAMI WAZUA GUMZO MTANDAONI, ADAIWA ANA UJA UZITO WA ARROW BOY

Nyota wa muziki nchini Nadia Mukami anadaiwa kushika ujauzito wa mpenzi wake Arrow Boy

Uvumi huo umeanza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii kutokana na muendelezo wa picha na mavazi ambayo Nadia Mukami amekuwa akivaa kwa sasa.

Kwanza kabisa ni picha aliyopiga na Arrow Boy ambayo inamuonesha  Nadia Mukami kuficha tumbo lake mbele ya camera jambo ambalo si kawaida yake.

Haijaishia hapo, vazi ambalo  Nadia Mukami alilivaa juzi kati akimsuprise mpenzi wake Arrow Boiy uraiani baada ya kutoka hospitali limefanya watu kupigia mstari kuwa mrembo huyo ni mjamzito kwani alikuwa amevaa nguo kubwa (Oversize)

Ikiwa ni kweli  Nadia Mukami ana ujauzito kwa sasa, basi huyo atakuwa mtoto wa kwanza kwa staa huyo mwenye umri wa miaka 26 na mchumba wake Arrow Boy

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke