Mwanamuziki kutoka Nigeria Teni The Entertainer anatuhumiwa kumtuma mlinzi wake ampige shabiki mmoja kwenye onesho lake lililofanyika nchini Nigeria.
Shabiki huyo anadaiwa kuwa alisikika akisema, siku hizi Teni hataki kupiga picha na mashabiki zake kwa sababu tayari ametoboa Kimuziki.
Kauli hiyo inadaiwa kumkasirisha Teni ambaye alikuwa Jukwaani na kumtuma mlinzi wake amshushie kipigo Jamaa huyo kiasi cha kumtoa damu kwenye Jicho lake la kushoto.