You are currently viewing Mwanamuziki kutoka Uganda Lydia Jazmine afunguka kupotea kimuziki

Mwanamuziki kutoka Uganda Lydia Jazmine afunguka kupotea kimuziki

Msanii wa kike kutoka nchini Uganda Lydia Jazmine amefunguka sababu za kutofanya vizuri kimuziki mwaka 2022.

Kwenye mahojano yake hivi karibuni amesema aliamua kuweka kila kitu pembeni kwa ajili ya kujitathmini na pia amekuwa akiendeleza biashara zake kimya kimya.

Mrembo huyo pia amedai kwamba mgogoro ulioibuka kati yake na uongozi  wake wa zamani ulilemaza juhudi za kuupambania muziki wake.

Hata hivyo amesema mwaka 2023 anarudi na kishindo kwenye muziki wake kwani ana mpango wa kuachia nyimbo mfululizo bila kupoa.

Utakumbuka Lydia Jazmine alivunja mkataba na meneja wake wa zamani Ronnie Mulindwa kutokana na migogoro ya kifedha lakini kwa sasa anafanya kazi kwa ukaribu na prodyuza Bushingtone.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke