Nyota wa muziki nchini Tanzania na mmiliki wa record label ya Konde Gang Harmonize amefanikiwa kufikisha jumla ya streams million 50+ katika mtandao wa boom play music Tanzania.
Kwa streams hizo Konde Boy anaungana na wanamuziki wengine wenye zaidi ya streams 50+ katika mtandao huo kama Diamond Platnumz ,Mbosso na Rayvanny ambaye ndiye kinara wa streams Afrika Mashariki.
Mpaka sasa mkali huyo wa ngoma ya “Teacher’ ametoa Album mbili ambazo ni Afro East ya mwaka 2020 yenye streams million 2.7 na Highschool ya 2021 yenye streams million 19, na EP moja ‘ inayokwenda kwa jina la Afro Bongo.