You are currently viewing MWANAMUZIKI WA UGANDA RAY G AMPOTEZA BINTIYE WA SIKU 12

MWANAMUZIKI WA UGANDA RAY G AMPOTEZA BINTIYE WA SIKU 12

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Ray G, ametangaza kumpoteza binti yake Kim aliyekuwa na umri wa siku 12.

Kupitia mitandao yake ya kijamii Ray G , amesema mtoto huyo alifariki Disemba 21 kufuatia kusumbuliwa na ugumu wa kupumua.

Msanii huyo amedokeza kwamba walifanya kila kitu kuokoa maisha ya binti yake huyo lakini juhudi zao ziliambuliwa patupu.

Kim alikuwa mtoto wa pili kwa Ray G na alimpata na mrembo Annabell Twinomugisha.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke