You are currently viewing NADIA MUKAMI AFUNGUKA KUHUSU SAFARI YAKE YA KUWA MAMA

NADIA MUKAMI AFUNGUKA KUHUSU SAFARI YAKE YA KUWA MAMA

Msanii nyota nchini Nadia Mukami amefunguka tusiyoyajua kuhusu safari yake ya kumlea na kumnyonyesha mtoto wake wa kiume Hasib Kai ambaye ana umri wa miezi miwili.

Katika kikao cha maswali na mashabiki zake kwenye mtandao wa Instagram Nadia Mukami amesema ameongeza uzito kutoka kilo 55 hadi 63 jambo ambalo amedai limechangiwa na yeye kula chakula kingi ili aweze kumnyonyesha mtoto wake bila kizingiti.

Mbali na hayo hitmaker huyo wa ngoma ya “Zawadi” ameweka wazi baadhi ya vitu ambavyo alikuwa hapendi alipokuwa  mjazito kwa kusema kwamba hakuwahi vutiwa na nyama ya ngombe, maziwa pamoja na mkate.

Hata hivyo kauli ya Nadia Mukami imezua hisia mseto miongoni mwa mashabiki zake ambapo wengi wamempongeza kwa hatua ya kumpa mtoto wake kipau mbele kwenye malezi tofauti na wanawake wengi  ambao hawapendi kuwanyonyesha watoto wao kwa ajili ya kulinda urembo wao.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke