You are currently viewing NANDY ATHIBITISHA KUFUNGWA KWA AKAUNTI YAKE YA INSTAGRAM

NANDY ATHIBITISHA KUFUNGWA KWA AKAUNTI YAKE YA INSTAGRAM

Staa wa muziki wa Bongofleva Nandy amethibitisha rasmi kuwepo na shida kwenye akaunti yake rasmi ya mtandao wa Instagram ambayo ina followers milioni 6.3

Kwa mujibu wa nyanzo vya habari za burudani kutoka nchini Tanzania, akaunti ya msanii huyo imekuwa disabled (imefungwa) na Instagram wenyewe baada ya jaribio la kudukuliwa na mtu ambaye bado hajafahamika.

Hata hivyo duru za kuaminika zinasema uongozi wake upo kwenye hatua za kuirejesha akaunti hiyo.

Utakumbuka kando na kujitangaza, miaka ya hivi karibuni akaunti za mastaa wa muziki zimekuwa moja ya vyanzo vyao muhimu vya kipato na wale wenye followers wengi wamekuwa wakipata deals zenye hela nyingi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke