You are currently viewing NASHA TRAVIS AKIRI KIKI INA MCHANGO MKUBWA KWA WASANII

NASHA TRAVIS AKIRI KIKI INA MCHANGO MKUBWA KWA WASANII

Msanii Nasha Travis amedai kuwa kiki zinaweza kuwa na mchango fulani katika muziki wa msanii tofauti na watu wengi ambao hupinga suala hilo.

Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Nasha amesema anaona ni sawa tu kwa wasanii kutengeneza matukio ili wazungumziwe mtandaoni kwani inasaidia kwa kiasi kikubwa kuinua muziki wao.

Katika hatua nyingine Mrembo huyo ambaye anafanya vizuri na single yake mpya “Naiwe” amesisitiza kuwa ingawa kiki ina mchango kwenye muziki, inapaswa kufanywa kwa ustaarabu kwani inaweza kuwa shubiri pale wasanii wanapotupiana maneno machafu mtandaoni.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke