You are currently viewing NAY WA MITEGO AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA

NAY WA MITEGO AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA

Msanii wa Hiphop kutoka Tanzania Nay wa Mitego ameachia rasmi album yake mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki zake.

Hitmaker huyo  wa ngoma ya “Atakuoa Nani” amewabarki mashabiki zake na  “Rais Wa Kitaa Album” ambayo ina jumla ya nyimbo 14 za moto, ikiwa na kutoka kwa wakali kama Alikiba, Marioo, Jux, Mejjah, Maua Sama, AY, Shammy, Runtown na Kelechi Africana.

Album hiyo ambayo ni ya kwanza kwa mtu mzima Nay wa Mitego tangu aanze safari yake ya muziki kwa sasa inapatikana kwenye majukwaa yote ya ku-stream muziki mtandaoni.

Utakumbuka mapema wiki hii iliyopita Nay wa Mitego alitajwa kuwania tuzo ya AFRIMA 2022 huko Nigeria kupitia vipengele viwili,  Best Artist Of The Year na Song Of The Year.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke