You are currently viewing Nay wa Mitego adai wasanii wengi Tanzania wanatumia dawa za kulevya

Nay wa Mitego adai wasanii wengi Tanzania wanatumia dawa za kulevya

Mwanamuziki wa Hip Hop kutoka Tanzania, Nay wa Mitego amedai kuna wasanii wengi kwa sasa wanatumia dawa za kulevya ila bado hawajajulikana.

Kupitia Insta Story amesema kama kuna la kufanya kupambana na hali hiyo ni sasa kabla mambo hayajawa mabaya zaidi.

“Kwenye music industry kuna tatizo kubwa la wasanii kujiingiza kwenye matumizi ya dawa za kulevya, now days imekuwa too much, yaani ni fashion, yaani wanaona ndio unyamwezi” amesema.

“Ni vile tu bado hawajafikia hatua mbaya na kugundulika kufuatana na madhara ya dawa. Tahadhari kubwa kabla ya hatari, kama kuna cha kufanya ni sasa kabla ya janga” amesema Nay wa Mitego.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke