You are currently viewing NI RASMI SASA RIHANNA ANA UJA UZITO WA MPENZI WAKE ASAP ROCKY

NI RASMI SASA RIHANNA ANA UJA UZITO WA MPENZI WAKE ASAP ROCKY

Ni Rasmi sasa mwanamuziki kutoka nchini marekani Rihanna ni mjamzito.

Mwimbaji huyo ambaye pia ni mwanamitindo anatarajia mtoto wake wa kwanza na rapa Asap Rocky.

Tovuti mbali mbali za nchini Marekani zimeripoti taarifa hii kufuatia picha ambazo zimewaonesha wawili hao wakiwa matembezini mjini New York wikendi iliyopita.

Mwaka 2019 ziliibuka taarifa kama hizi lakini alizikanusha kwenye mahojiano na Jarida la Vogue.

ASAP Rocky na Rihanna wamekuwa marafiki wa karibu katika kipindi cha muda mrefu kabla ya kuthibitisha hadharani kuwa wanapendana mwaka wa 2021.

Mwaka wa 2013, Rihanna alitokea katika video ya Asap Rocky ya “Fashion Killa” kama video vixen,jambo ambalo lilihusisha uwepo wa mahusiano ya kimapenzi kati yao.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke