You are currently viewing Nitawaunganisha wasanii wa Uganda na waandaaji wa Grammy -Eddy Kenzo

Nitawaunganisha wasanii wa Uganda na waandaaji wa Grammy -Eddy Kenzo

Mwanamuziki Eddy Kenzo ameahidi kuwaunganisha wanamuziki wengine wa Uganda na waandaaji wa tuzo za Grammy pindi atakapohudhuria hafla ya utoaji wa tuzo hizo mwakani nchini marekani.

Kwenye mahojiano yake hivi karibuni, Kenzo amebainisha kuwa kuteuliwa kwenye tuzo za Grammy 2023 itawafungulia milango wasanii wengi nchini humo kuupeleka muziki wao kimataifa na kushiriki tuzo kubwa duniani .

“Nataka kwenda Marekani na kukutana na watu hawa. Nataka kuwajua ili niweze kuwaunganisha na wanamuziki wa Uganda. Nataka kufungua mlango kwa kila mtu,” alisema Eddy Kenzo.

Eddy Kenzo ametajwa kuwania Tuzo za Grammy mwaka 2023 kupitia kipengele cha Best Global Music Performance na wimbo wake ‘Gimme Love’ aliomshirikisha Matt B.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke