Rapa Noti Flow ameweka wazi namna mpenzi wake King Alami anaendelea hospitali mara baada ya kupata majeraha mabaya alipojirusha kutoka kwa jumba la ghorofa 7.
Kupitia instastory yake amesema mrembo huyo anaendelea kupata nafuu na huenda madaktari wakamruhusu kurudi nyumbani hivi karibuni.
Lakini pia amewataka mashabiki kumpa nafasi King Alami pindi atakaporejea kwenye mitandao ya kijamiii.
Ikumbukwe kisa cha Kinga Alami kujirusha kutoka kwa jumba la ghorofa saba kisa kukataliwa na Noti Flow lilimpelekea kupoteza mkono wake wa kulia huku goti lake la mguu wa kulia likivunjika.