You are currently viewing Noti Flow ajutia kuvunja uhusiano wake na King Alami

Noti Flow ajutia kuvunja uhusiano wake na King Alami

Mwanamuziki mwenye utata nchini Noti Flow amekiri kuumia na kujutia kitendo cha kuvunja mahusiano yake na aliyekuwa mpenzi wake, King Alami.

Kupitia ukurasa wake wa instagram Noti flow amesema mahusiano yao hayangevunjika huenda tukio la king alami kutaka kujiua kwa  kujirusha kutoka kwa jumba la ghorofa tano alingefanyika.

Aidha amefichua kuwa watu wengi mitandaoni wanamlaumu kuwa yeye ndio chanzo cha kisa hicho kutokea huku akisema kuwa jumbe hizo zimemfanya ajihisi vibaya zaidi kwa hatua ya kumkimbia mrembo huyo ambaye walikuwa wanashiriki pamoja mapenzi ya jinsia moja.

“We gon pray for you my baby We’ve been praying for you day & night . You’re strong my G & you’re still the coolest stud I fell in love with I love you more everyday Nothing’s changed & I’m with you thru it all.. I’m here for you forever my love. Quick recovery my baby you are loved and cherished ( for those who are blaming me thank you very much for making me feel worse & guilty than I already I’m. Y’all are right tho, it’s my fault cz if I was with her she’d be OK & safe like she’s always been so crucify me”. Ameandika

Kauli yake imekuja siku moja baada ya kuwaomba wafuasi wake wamsaidie kuchangisha pesa za kugharamia matibabu ya aliyekuwa mpenzi wake, King Alami ambaye kwa sasa bado amelazwa katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke