Staa wa muziki wa Bongofleva, msanii Ommy Dimpoz amefanikiwa kushinda tuzo kutoka kwenye jukwaa kubwa la mitindo Afrika Mashariki na Kati la Swahili Fashion Week lililofanyika katika Hoteli ya Serena, Jijini Dar es salaam.
Tukio hilo kubwa zaidi la mtindo hufanyika kila mwaka na mwaka huu wa 2021, Ommy Dimpoz ametajwa kushinda tuzo ya ‘Male Stylish Personality of the Year 2021’.
Kwenye kipengele hicho alichoshinda ommy Dimpoz, alikuwa akishindana wakali wengine kama;, Rich Mitindo, Jimmy Chansa, Quick Rocka, Maxi Rioba na Jamal April.