You are currently viewing Otile Brown afunguka kuhusu kujipendekeza kwa mpenzi wake wa zamani Nabayet

Otile Brown afunguka kuhusu kujipendekeza kwa mpenzi wake wa zamani Nabayet

Staa wa muziki nchini Otile Brown amewajibu wanaodai kuwa anajipendekeza kwa mpenzi wake wa zamani Nabayet licha ya mahusiano yao kuvunjika.

Otile ambaye amerejea nchini baada ya kukamilisha ziara ya miezi miwili nchini marekani amewashangaa wanaomsema vibaya kuwa bado anamzimia kimapenzi mrembo huyo kwa kusema kuwa hajutii kitendo cha kumtumia salamu za heri kwenye kumbukizi ya kuzaliwa kwake kwani ni moja kati ya watu ambao anawapenda sana.

Otile Brown na Nabayet walikuwa kwenye mahusiano kwa kipindi cha miaka miwili lakini mahusiano yalikuja kuvunjika mwaka wa 2020 kutokana na umbali kati yao.

Utakumbuka mwaka wa 2019 Otile Brown aliachia wimbo wa kusifia urembo wa Nabayet baada ya penzi lao kunoga.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke