You are currently viewing OTILE BROWN APOKEZWA TUZO YA DHAHABU NA YOUTUBE KWA KUFIKISHA SUBSCRIBERS MILIONI 1.

OTILE BROWN APOKEZWA TUZO YA DHAHABU NA YOUTUBE KWA KUFIKISHA SUBSCRIBERS MILIONI 1.

Staa wa muziki wa nchini  Otile Brown amepokezwa tuzo ya Golden creators na mtandao wa youtube kwa kufikisha jumla ya subscribers millioni 1.

Mkali huyo wa “Jeraha” amewashukuru mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuendelea kufuatilia kazi zake ambazo zinaendelea kuonyesha mafanikio makubwa huku akiahidi kutoa mzuri kwa ajili yao .

Otile Brown anakuwa msanii wa kwanza kutokea Kenya kuwa na wafuasi wengi zaidi katika mtandao wa YouTube huku Dusuma aliyomshirikisha Meddy ikiwa ndiyo video yenye watazamaji wengi zaidi ikiwa na views milioni 35 ndani ya mwaka mmoja.

Baadhi ya wasanii kutoka Kenya wanaofuata kwa wafuasi wengi ni pamoja na Bahati Kenya  akiwa na subscribers elfu 902K, Willy Paul 877K, Sauti Sol  856K,  Khaligraph Jones 538K, na Nyashinski 473K.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke