You are currently viewing PHILLIPPE COUNTINHO AJIUNGA NA ASTON VILLA KWA MKOPO TOKA BARCELONA

PHILLIPPE COUNTINHO AJIUNGA NA ASTON VILLA KWA MKOPO TOKA BARCELONA

Kiungo wa kimataifa wa Brazil na Barcelona Philippe Coutinho atajiunga na Aston villa Kwa mkopo hadi, mwisho wa msimu.

Vilabu vya Aston Villa na Barcelona vimekubaliana juu ya uhamisho wa nyota huyo na villa watalazamika kulipa sehemu ya mshahara wake.

Inatajwa kuwa Kiungo huyo ameshawishika zaidi kujiunga na Villa kutokana na Meneja wa Klabu hiyo Steven Gerrard kwa sababu walicheza wote Liverpool.

Kiungo huyo mshambuliaji mwenye umri wa miaka 29 aliichezea Klabu ya Liverpool kwa miaka mitano (2013-18) kisha kujiunga na Barca ambayo aliitumikia kwenye michezo 76 kisha kutolewa kwa mkopo katika Klabu ya Bayern Munich na sasa Aston Villa.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke