You are currently viewing Prodyuza Bobix amshutumu Bebe Cool kwa wizi wa beat ya wimbo

Prodyuza Bobix amshutumu Bebe Cool kwa wizi wa beat ya wimbo

Mwanamuziki Moses Ssali maarufu Bebe Cool kwa mara nyingine tena amegonga vichwa vya habari kwa tuhuma za kuiba mdundo wa wimbo wake mpya uitwao ““Don’t Stop”.

Kulingana na mtayarishaji wa muziki aitwaye  Bobix Pro ameumizwa na kitendo cha bosi huyo wa Gagamel kutumia kazi yake bila idhini.

Mtayarishaji huyo maarufu anadai Bebe Cool na watayarishaji wake, walitumia ubunifu wake wa kisanii katika wimbo wao mpya huku akidai alivunjika moyo alipotazama video hiyo na hakutajwa sehemu yeyote.

Bobix ameongeza kuwa hakutambuliwa na Bebe Cool kwani nembo yake iliyokuwa kwenye wimbo huo iliondolewa kwa njia ya kujaribu kuharibu ushahidi unaoonyesha wimbo huo ni wake.

Alipowasiliana na Bebe Cool kuelezea masikitiko yake kuhusu wimbo wake mpya kupitia GreenApp, Bebe Cool aliahidi tu kurekebisha makosa yake kupitia ukurasa wake wa Facebook atakapoanza rasmi kutangaza wimbo huo.

Mtayarishaji Bobix hakuridhishwa na maelezo ya Bebe Cool kwani alishangaa itamsaidia vipi kwani wimbo huo tayari umeanza kupigwa kwenye vituo tofauti vya redio na televisheni nchini Uganda.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke