You are currently viewing PUSHA T AFUNGUKA SABABU ZA KUMALIZA UGOMVI WAKE NA DRAKE

PUSHA T AFUNGUKA SABABU ZA KUMALIZA UGOMVI WAKE NA DRAKE

Rapa kutoka Marekani Pusha T hatimaye amefunguka sababu iliyomfanya kumaliza bifu yake na Drake ambayo ilidumu kwa miaka 10.

Kwenye mahojiano na Desus & Mero, Pusha T ameeleza kwamba, kuwa Baba mwaka 2020 ndio sababu pekee iliyomfanya aimalize bifu yake na Drizzy kwani kulimbadilisha mtazamo wake kwa ujumla hasa kuwahusisha watoto kwenye ugomvi.

Kama utakumbuka vyema, Pusha T ndiye aliifahamisha dunia kwamba Drake ana mtoto anaitwa Adonis lakini alimficha.

Kupitia freestyle yake ‘The Story of Adidon’ Pusha alichana “You are hiding a child, let that boy come home/ Deadbeat mothaf*cka, playin’ border patrol/ Adonis is your son.”

Hii ilimfanya Drake na baadaye kuthibitisha taarifa hizo kupitia album yake, Scorpion mwaka 2018.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke