Rapa kutoka Kenya Kaa la Moto ametangaza ujio wa album yake mpya ambayo ana mpango wa kuachia ndani ya mwaka 2022.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram Kaa La Moto ametusanua kuwa album yake mpya ambayo anaianda chini studio za Kubwa Studios mjini mombasa imekamilika kwa asilimia 90 kabla ya kuingia sokoni.
Licha ya kutoweka wazi jina la album yake mpya, rapa huyo pia hajatuambia idadi ya ngoma pamoja wasanii watakaoshirikishwa kwenye album hiyo ila ni jambo la kusubiriwa.
Hii itakuwa ni album ya pili kutoka kwa mtu mzima Kaa La Moto baada ya kesi ya mwaka wa 2019.