You are currently viewing RAPPER LIL DURK AWATAHADHARISHA WANAOTAKA KUACHIA KAZI ZAO IJUMAA HII

RAPPER LIL DURK AWATAHADHARISHA WANAOTAKA KUACHIA KAZI ZAO IJUMAA HII

Rapa kutoka Marekani Lil Durk amewapa tahadhari wasanii wanzake ambao nao wanamipango ya kuachia kazi zao mpya ijumaa ya wiki hii.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram rapa huyo ambaye ni mzaliwa wa Chicago, Illinois ameweka wazi kuwa album yake ya “7220” haita ahirishwa tena na yeyote atakayetaka kuachia album yake Machi 11 mwaka huu ajipange kwa kuwa amejipanga kuuza zaidi ya wote watakaoachia album siku hiyo

Hayo yanajiri ikiwa ni wiki kadhaa zimepita tangu asogeze mbele tarehe ya kuachia album yake mpya iitwayo “7220” ambayo ilikuwa itoke Februari 22, tarehe moja na album ya Kanye West, akakubali yaishe akasogeza mbele album yake.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke