Mshindi pekee wa tuzo ya BET Tanzania na Mkurugenzi wa lebo ya Next Level Music Rayvanny ameachia EP yake mpya inayokwenda kwa jina la NEW CHUI.
Rayvanny ameamua kuwa surprise mashabiki zake kwa kuachia EP hiyo mpya yenye nyimbo sita huku ikiwa na kolabo moja tu ya Abby Chamz.
Hii inakuwa EP ya pili kutoka kwa mtu mzima Rayvanny baada ya ile ya kwanza Flowers aliyoiachia February 28,mwaka wa 2020 kufanya vizuri kwenye Digital Platforms za kusambaza muziki duniani.
Mpaka sasa Rayvanny anajumla ya EP mbili na Album moja ambayo ni Sound from Africa iliyotoka mwaka huu 2021.