Nyota wa muziki wa Bongofleva Rayvanny anaendelea kugonga vichwa vya habari kuhusiana na STREAMS za kazi zake mtandaoni.
Good news ni kwamba Rayvanny amefanikiwa kufikisha jumla ya STREAMS Milioni 100 kwenye App namba moja ya kusikiliza na kupakua muziki mtandaoni ya Boomplay Music.
Bosi huyo wa lebo ya Next level Music anakuwa msanii wa kwanza Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kufikia idadi hiyo kubwa ya streams.
Aidha, kwa Tanzania anayemkaribia Rayvanny kuwa na idadi kubwa ya streams ni Diamond Platnumz ambaye hadi sasa ana zaidi ya streams Milioni 90.3.